Monday, December 31, 2012

MAANDAMANO YA MTWARA JANA KUHUSU KUPINGA KUSAFIRISHWA GASI YA MTWARA KENDA DAR ES SALAAM INATOA FUNDISHO GANI?

MAANDAMANO YA MTWARA JANA KUHUSU KUPINGA KUSAFIRISHWA GASI YA MTWARA KENDA DAR ES SALAAM INATOA FUNDISHO GANI?


MAANDAMANO YA MTWARA JANA KUHUSU KUPINGA KUSAFIRISHWA GASI YA MTWARA KENDA DAR ES SALAAM INATOA FUNDISHO GANI?
MAKALA TIME NA CHIWAMBO
Jana nchi nzima imepata habari juu ya maandamano yaliyotokea Mkoani  Mtwara kuhusu kupinga kusafirishwa kwa gesi yao kupelekwa jijini Dar es salaam. Kwa wale waliokosa kuangalia televisheni, Radio au kupata taarifa kwenye tovuti mbalimbali basi leo asubuhi walipata kusikia juu ya maandamano hayo kupitia magazeti ya leo asubuhi.
Swali la kujiuliza ni kwamba kwanini maandamano yametokea? Kwa nini hii ni mara ya pili kwa mtwara kuandamana ndani ya mwaka mmoja? Tatizo kubwa ni nini? Je wametimiziwa mahitaji yao kwanza kabla gesi yao haijaanzwa kuchimbwa? Kwa maana hiyo watu wengi wanaofuatilia masuala ya kitaifa na mustakabali wa Taifa letu basi atakuwa amejiuliza maswali mengi sana pengine ni tofauti na maswali yangu.
Baadhi ya Mabango yalisema “Ukiiuuaa! Tunakupeleka The Heg Gesi Haitoki, Mshua hii Gesi ni ya wamakonde tafuta ya Wakwere, Mh. Kikwete Tatizo sio Gesi Mikataba yako Noma, Gesi Kwanza Uhai Baadae, Bandari Bagamoyo Gesi Bagamoyo Viwanda Bagamoyo Mtwara wapuuz,  na linguine lilisema Gesi Ibaki au Tugawane Nchi”. Hayo ni baadhi tu ya Mabango jinsi yanavyoonyesha.
Hapa kwa sisi tuliosomea au tunaosomea masomo ya Jamii tunabaini kwamba hapo pana tatizo. Wananchi inawezekana hawajatimiziwa mahitaji yao. Kutokana na hali hiyo iliwafanya wao waandamane. Hii ni hatari kwa nchi yetu. Tukiangalia kwa undani zaidi kuhusu suala la kuwapunguzia gharama za umeme kwa wakazi wa Mtwara hiyo bado sio suruhu la matatizo ya wananchi.
Kwa kiasi kikubwa maeneo ya kusini ukianzia mkoa wa Lindi, Mtwara, na Kumalizia Ruvuma hali ya wananchi ya maendeleo ni Mbaya sana ten asana. Watu walio wengi wanaonyesha wamekata tama na mfumo wa maisha wanayoishi. Mwezi  Julai Mwaka huu nilikuwa wilaya ya Newala katika sehemu za tafiti zangu za kuizunguka Nchi yetu hasa maeneo ya vijijini.
Nyumba za wananchi wengi huko ni za Nyasi hasa vijijini. Je kuwaambia hawa watu kuwa watapunguziwa gharama za umeme wakati wanaishi nyumba za nyasi inakuja akilini kweli? Kwanini hali hii unadhani kwa nini wananchi hao  waliandamana. Zao kuu walilokuwa wanategemea kulima na kuuza ili waendeshee maisha yao ni Korosho. Hili ni zao ambalo uuzaji wake sasa unaleta wasiwasi kwa wananchi na walio wengi sasa wamekata tama kulimia hasa wale wakulima wadogo wadogo.
Kama serikali ingeboresha zao la korosho hawa wananchi wangeweza kununua bati na vifaa vingine vya ujenzi ili wapate kunufahika na punguzo la Gharama  za umeme kwa wanamtwara. Hivi mwananchi atawezaje kuweka umeme kwenye nyumba ya nyasi? Wakati huu sasa sio wa kuwadanganya wananchi. Mufanye tafiti kule vijijini kusini mwa Tanzania mutaona hali ilivyo ya kimaisha. Watu walio wengi wanaishi majumba ya majani au Nyasi kipindi kingine wengine hujenga nyumba zinazoitwa suti yaani Nyasi chini hadi juu. Eti tumwekee umeme mtu huyu inakuja akilini?
Tuangalie namna ya kutatua matatizo ya wananchi. Je wananchi wamepewa nafasi ya kusikilizwa? Je wao mapendekezo yao yanesemaje? Je timu ya washauri ilikwenda huko? Mambo mengine hayana haja ya Rais wan chi aingilie kati. Viongozi wa chini wamewajibika vipi kuwalainisha wananchi ili waweze kuruhusu gesi yao ipelekwe Dar es salaam.
Ni Matumaini yangu kuwa utaweza kukaa na kutafakari zaidi wewe Mtanzania kwamba kifanyike nini ili kuzuia maandamano ya wananchi kila kukicha. Kuna mtu alikuwa anatania eti kwa sasa pamefikia mahari hata watoto nao wanaweza kuandamana kumshinikiza baba awe anarudi nyumbani mapema. Why?
Maoni yako Tima Kwa barua pepe au hapo chini ausichiwambor@hotmail.com

No comments:

Post a Comment